Labels

Saturday 30 September 2017

UFUGAJI WA SAMAKI

Aina ya samaki wafugwao ni perege, sato ngege, magenge nk. Sababu za kufuga samaki  wa jami hizo ni ;
  1.  Huishi katika maji ya kawadia yenye joto la wastani 
  2. Huzaliana kwa wingi
  3. Hula majani ambayo hupatikana kiraisi majumbani na mashambani 
       MAHITAJI KATIKA UFUGAJI WA SAMAKI

  1. Uchaguzi wa eneo
  2. Uchimbaji wa bwawa
  3. Mbolea na majivu
  4. Uwekaji wa maji
  5. Upendaji wa vifaranga
  6. Usafishaji wa bwawa
      UCHAGUZI WA ENEO

  1. Pasiwe na mteremko mkali
  2. Pawe na udongo unaohifadhi maji
  3. Pawe na maji ya kudumu
  4. Pawe karibu na nyumbani
     UCHIMBAJI WA BWAWA
  1. Safisha eneo kisha lipime kulingana na ukubwa wa mahitaji ya bwawa lako
  2. Pima kingo weka kamba kuonyesha sehemu kingo zako zitakapopita
  3. Chonga sakafu yako chini na  sawazisha kuta zote za juu.
  4. Panda majani ya mudu ili kuzuia mmomonyoko

Friday 29 September 2017

MALIGHAFI ZAKUTENGENEZA CHAKULA BORA CHA KUKU WA NYAMA(BROILER)

  1. MAHINDI.
  2. MASHUDU YA ALIZETI(mabaki ya alizeti baada ya kuondolewa mafuta)
  3. Mashudu ya pamba.
  4. Dagaa.
  5. Damu.
  6. Pluard.
  7. Pumba ya mashudu.
  8. Lime store.
  9. mifupa
  10. chumvi.
  11. Premix.
JINSI YA KUTENGENEZA CHAKULA CHA KUKU BORA WA NYAMA(BROILER).
  1. Mahindi-200kg-100kg.
  2. Mashudu ya alizeti-40kg-20kg.
  3. Dagaa-35kg-20kg.
  4. Damu-19kg-10kg.
  5. Pluard-65kg-35kg.
  6. Pumba ya mashudu 55kg-30kg.
  7. Lime store 25kg-20kg
  8. Mifupa 10kg-5kg.
  9. chumvi 2kg-2kg.
  10. Premix 2kg-2kg.
Waweza kuchanganya mchanganyiko huu kiasi chochote unacho weza zingatia kanuni yaani maelezo ya msingi.

GROWER MASHI
CHAKULA CHA KUKU
Mahindi    -165kg-85kg.
Pumba       -35kg-20kg
Dagaa        -35kg-50kg
pumba       -80kg-45kg
Mifupa       -7kg-5kg
Alizeti        -55kg-25kg
Chokaa       -25kg-13kg
Chumvi      -1.5kg-1.5kg
Premix      -2kg-2kg
Rice polish -85kg-45kg.

CHICK MASH BROFER,LAYER'S,KIENYEJI.
Mahindi -27kg-140kg.
Pumba   -27kg-25kg.
Mifupa  -7kg-25kg.
Alizeti    -75kg-48kg chokaa 1.5-1kg.
Chumvi  -2kg-1kg
Premix   -1kg-1kg.
Lysine    -0.6-0.3kg
Dop 1 meth 10 mine-0.6kg-0.4kg.

Friday 22 September 2017

UFUGAJI WA KUKU.


Kuku wa kienyeji.
kujenga banda lakuku.
Unavyoanza kujenga banda la kuku kitu cha kwanza kupangilia mpangilio mzima wa mabanda yatakayo kaa:
  • Upepo.
  • Sehemu iwe inafikika
  • Na isiwe na unyevunyevu.
Mpangilio wa mabanda. 
Banda la kwanza kabisa ni banda la kuku wa nyama ndio lina jengwa mwanzoni,kuwe na upepo wa kutosha na banda linalo fuata ni kuku wa mayai,banda la mwisho kabisa ni banda la kuku wa kienyeji hili lina jumuisha bata,bata mzinga pamoja na kanga na ndege wengine wafugwao
sababu zinazo fanya ujenzi huu wa banda bora uwe wa mpangilio ni hizi zifuatazo;

(1) Magonjwa mengi ya kuku yana ambukizwa kwa njia ya hewa hivyo huwauwa zaidi kuku wa nyama wanao wahi kutoka bandani  ni rahisi kupata maambukizi kutoka kwenye kuku wanao kaa mdamrefu bandani.

(2)Kwamfano kuku wa kienyeji,bata,bata mzinga,kanga hukaa bandani mda mrefu sana hivyo magonjwa ya kuambukiza huwa wana kaanayo sana mwilini mwao kwaiyo wao wanakua wamejijengea kinga mwilini mwao tofauti na kuku wa nyama.

ULISHAJI WA KUKU WA KIENYEJI.














1)Kula kwa kuzurura(free range system)
2)kula kwa kufungwa/kwenye mabanda.

1)Njia ya kuzurura.
Kuku wanaofunguliwa tu na kuanza kutafuta chakula wenyewe njia hii ni rahisi lakini kutoa dawa kwa kulisha ni ngumu kwasababu kuku wanapo rudi jioni huwa wameshiba hivyo huwezi wapa dawa kirahisi.
2)Njia ya kufugia kwenye banda.
Njia hii ni nzuri lakini ina madhara kwa mfugaji asiye makini kwasababu inaitaji uangalizi mzuri katika kulisha chakula kwani  virutubisho vingi vya kwenye chakula kuku anaye zurura anauwezo wa kujitafutia mwenyewe nakuweka uwiano wa virutubisho ndani ya mwili wenyewe.
  KUZUIA MAGONJWA YA KUAMBUKIZWA WENYEWE KWA WENYEWE

1)MABORESHO YA UFUGAJI.
     Kwakawaida kuku wa kienyeji huchukua miezi 5-6 kuanza kutaga mayai lakini chakula bora kimefuta mfumo huo hivyo kuku wakienyeji sikuizi huchukua miezi mi 4 na kuanza kutaga,kama utafuata ufugaji bora na chakula bora hutaga mayai 100 kwa mwaka.
 MABANDA.
         Mabanda yawe na hewa ya kutosha ili waweze pumua vizuri bila kushikana.
2)Waweza weka bembea ndani ya nyumba huwafanya kuku mifupa itanuke kila wanapo ruka ni mazoezi ya kujenga mwili.
3)AINA MBILI ZA KUFUGA KUKU WA/NDANI(INTENSIVE SYSTEM)
1)Berry charge system(ufugaji wa kutumia vyuma au mbao).
2)Deep litre system.
Njia ya kulisha kuku katika banda tunatakiwa maranda,majani ya mpunga/ngano,Pumba hutumika kiasi cha 12.20 za ujazo.

FAIDA ZAKE.
-Kuku wengi hufugwa katika sehemu ndogo.
-kuku hupata kinga za hali ya hewa,jua na baridi.
 Pia hukingwa zaidi na wanyama wasumbufu kama mwewe,panya,nyoka.
-Mmayai hukusanywa zaidi.
-Kuku hufugwa zaidi kibiashara rahisi kulindwa magonjwa na wadudu.
-Mbolea hupatikana kwa wingi

ULEAJI BORA WA VIFARANGA
 Mambo mengi yana usika katika uleaji wa vifaranga.Uleaji hutofautiana kati ya vifaranga wa kuku wa mayai na kienyeji na kuku wa nyama katika lishe na chanjo.
MATAYARISHO
  •      Banda liwe imara kuepuka wizi wa wanyama wasumbufu kama nyoka,paka,mwewe na kunguru.
  •      Banda lijengwe sehemu yenye hewa safi ya kutosha na kavu isiyo na unyevu nyevu 
  •      Kabla ya kuingiza safisha banda nje na ndani kwa kutumia dawa yakuua vijidudu vya magonjwa.Paka chokaa kuta za ndani na hakikisha banda haliwi na joto kali,baridi kuingia,mvua na upepo mkali.
  • Tayarisha chakula bora na vifaa vya kulishia na kunyweshea maji,tandiko safi na dawa.

                               KABLA YA KUFIKA VIFARANGA

 Banda liwe tupu kwa wiki moja baada ya kusafisha kwa dawa.Vifaranga utakao pewa watoke kwenye mzalishaji mwenye historia nzuri.
  • Usichanganye vifaranga wa sehemu tofauti
  • Vifaranga hawawezi kuathirika haraka na mazingira hivyo ya faa kuwa na uangalifu wa hewa,mwanga na joto.
  • Vifaa vya mwanga na joto ni  muhimu na lazima katika kulea vifaranga.
  • Tangazi za mduara kwa kutumia hard yenye urefu wa cm 60 na katikati weka balbu au jiko la mkaa  na taa ya mafuta kisha mwanga wa kutosha ili vifaranga waone chakula na maji 
  • Weka chokaa halafu maranda tandika chilk paper au magazeti juu ya maranda.
  • Masaa matano kabla ya kufika vifaranga washa joto au jiko la mkaa kwaajili ya joto liwe la nyuzi linakuwa la wastani wiki ya 1-35 nyuzi joto. 
NB.Tumia maji ya mvua au ya bomba chemsha yapooze ili kuharibu chroline pia usitumie dawa ya kuua wadudu.
     Siku ya tatu kabla ya chanjo usitumie ant biotic  na siku tatu baada ya chanjo wasipewe antibiotic wapewe vitamin tu.
 Rudia chanjo ya new castle kila baada ya mieze mi tatu chanjo ya maleks hufanyika kwa mzalisha.(Hatchery).

TIBA KWA MINYOO
      Hii hufanyika kwenye kuku wa mayai mara ya  kwanza hupewa wiki 8-12 na hurudiwa kila bada ya miezi mi tatu.

KUKU WA NYAMA(BROILER)
Kuku wa nyama anatakiwa apate eneo la futi moja ya mraba.Nyumba iwe na madirisha ya kutosha,hewa safi ,sakafu iwe na godoro(LITTER) ya maranda ya mbao au maganda ya mpunga.

VIFAA
  Tayarisha vyombo vya chakula na maji yakutosha kulingana na idadi ya kuku.Vifaranga 100 wanaweza kutumia chombo kimoja cha kulishia(chick plate) na chombo kimoja cha kunweshea maji kwa wiki moja ya mwanzo.Wiki ya pili na kuendelea tumia feedr moja yenye kipimo chasentimita 38 kwa kuku 50 na chombo kimoja cha maji kwa kuku 60.

CHAKULA KINACHO TAKIWA.

UMRI(WIKI)                                                                AINA YA CHAKULA
 0-2                                                                                    CHICK STATER.
3-4                                                                                      BRILER FINISHER.