Labels

Thursday 12 October 2017

JINSI YA KUTENGENEZA SHAMPOO



 shampoo zipo za aina nyingi inategemea virutubisho na kemikali zilizotengenezwa.kuna shampoo ambazo zina harufu nzuri .kwa mfano waweza tumia perform[harufu]kama havened lemon,jasmine,peach apples) na shampoo za virutubisho kama parachichi,karoti alovera,tango,mayai.

Mfano(i)
Kutengeneza shampoo (ambayo inatumia chemical)
zilizochanganywa harufu au perfume(vyote ni kuchanganya kwa pamoja
na kukoroga tu).

Mfano(ii)
malighafi za shampoo isiyo na virutubisho/shampoo hiyo
unaweza tengeneza kwa formula mbili
.    sulphonics Acid
.    soda ash
.    maji
.    sless
.    rangi
.    perfume
.    grycelin
.    chumvi.

JINSI YA KUTENGENEZA:
HATUA YA 1.
Kwanza tayarisha malighafi zote,ziwe juu ya meza utakayo fanyia kazi,vyombo vya kufanyia viwe visafi na kumbuka kusafisha kwa maji kila unachotumia.
Tayari vifaa vya  kufanyia kazi
  • Anza na sulphonic acid vijiko (4) vya chakula tumbukiza kwenye ndoo au mashine yako.
  • Fuatia na soda ash vijiko(2) vya chai lakini kumbuka kuchanganya na maji kidogo.
  • Koroga na mwiko au na mti baada ya mchanganyiko 
  • Tia maji lita 4 nakuanzia hapo anza kukoroga kwa muda wa dakika kumi,kisha unafuatia malighafi zifuatazo
  • Strees-robo
  • Glycerine vijiko(3) vya chakula
  • Perfume-kijiko cha chai kimoja
  • Rangi-Kijiko cha chai kimoja.
  • Chumvi kijiko cha chai kimoja
   Usiweke kitu kingine na ukumbuke chumvi ni ya mwisho kama muda umefika ikiwa nzito kama uji/shampoo yako itakua tayari.

Monday 9 October 2017

JINSI YA KUTENGENEZA MANGO PIKO.

MANGO PICLES.










   
  • Mango picles ni (achari) au (appetizer) nzuri kwa asali ya chakula.
  • Malighafi kubwa zaidi ni embe bichi.

 MATAYARISHO.
  • Maembe ya safishwe vizuri kwa kuosha vizuri kwakutumia maji safi na maembe ya oshwe kabla hayaja menywa. 
  • Embe likatwe katwe vipande bila kugusa kokwa,Vipande ivyo viwekwe kwenye kichanja baada ya kukatwa na vianikwe juani kwa muda wa nusu saa.
  • Hifadhi embezako hizo kwenye chombo kisafi waweza acha humo kwa muda wa siku 5.
  • Kwamfano embe ulilonalo ni moja tayari viungo kama nyanya vitunguu,mafuta ya kupikia,chumvi.
KUTENGENEZA.
  • Tayarisha nyanya 1/2Kg,menya maganda na kukatakata vipande vidogo.
  • Katakata vitunguu vikubwa vi 2.
  • Chumvi vijiko viwili vya chai.
  • Kijiko kimoja cha chai kwaajili ya kuifanya mango piko yako isiharibike.
  • Maji ya limau vijiko 2 vya chai.
  • Tengeneza posti ya mchanganyiko huo.Baada ya kutayarisha(rosti)hiyo,chukua vipande vyako vya embe na kuchanganya na rosti hio.
  • Kwa rosti hii embe tumia moja lenye ujazo wa 1/4kg.
  • Weka kwenye chombo na ufunge mfuniko vizur acha kwa 3-4 siku.
  • kisha enjoy mango piko yako.

Monday 2 October 2017

KILIMO CHA UYOGA

Uyoga ni mmea ambao hauna ukijani,uyoga ni jamiiya fungi



AINA ZA UYOGA
  1. Uyoga taka 
  2. Uyoga tegemezi
  3. Uyoga ufaana
  4. Uyoga sumu
MAHITAJI KATIKA KUPANDA UYOGA
  1. Mbegu
  2. Banda la kupandia uyoga
  3. Vimeng'nywa
  4. Mifuko ya plastiki
Mbegu
Mbegu za uyoga hupatikana katika maduka ya kuuza mbegu si rahisi kwa mkulima kutengeneza mbegu hizo kwani huharibika upesi huchukua mwezi mmoja kuharibika

BANDA LA KUPANDA UYOGA
Banda lakupandia uyoga linakuwa na sehemu  kumi na mbili sehemu ya kupandia na sehemu ya kukuzia. Sehemu ya kupandia huwa na giza chumba chote na sehemu ya kukuzia huwa na mwanga hafifu kwani  uyoga wakati unaota unahitaji carbondioxide kwa wingi na oxigyen kidogo

VIMENG'NYWE
Vimeng'nywe ni mabaki ya takataka za mazao zinatumika katika kupanda uyoga mfano , mabua ya mahindi, maranda ya mbao pamba maganda ya ndizi n.k
takataka zote za mazao zinazooza zinafaa


JINSI YA KUANDA VIMENG'NYWE
Katakata vipande vidogovidogo tayari kwa kuvianda kama shamba lako
  • Kuandaa vimeng'nywe kwa njia ya kuvichemsha kwa kutumia gunia au kapu
  • Kuanda vimeng'nywe kwa kuvichemsha kwa mvuke ndani ya mifuko ya plastiki
AINA ZA UPANDAJI
  1. Kuchanganya mbegu na vimeng'enywa
  2. kupanda kwa tabaka
  3. Kusiha mbegu juuya vimeng'enywa
MIFUKO YA PLASTIKI
Mifuko ya plastiki ndio shamba lako la uyoga inatumika kuweka vimeng'enywa na kupandia uyoga,unaweka vimeng'enywa na kupanda mbegu kisha unafunga juu na kutoboa vitundu vitano vitano kwa kila upande unapeleka katika chumba cha kupandia baada ya wiki moja au mbili uyoga utakua umeota hivyo utahamisha katika chumba cha kukuzia chana mfuko wako kwa kutumia kisu.