Labels

Monday 2 October 2017

KILIMO CHA UYOGA

Uyoga ni mmea ambao hauna ukijani,uyoga ni jamiiya fungi



AINA ZA UYOGA
  1. Uyoga taka 
  2. Uyoga tegemezi
  3. Uyoga ufaana
  4. Uyoga sumu
MAHITAJI KATIKA KUPANDA UYOGA
  1. Mbegu
  2. Banda la kupandia uyoga
  3. Vimeng'nywa
  4. Mifuko ya plastiki
Mbegu
Mbegu za uyoga hupatikana katika maduka ya kuuza mbegu si rahisi kwa mkulima kutengeneza mbegu hizo kwani huharibika upesi huchukua mwezi mmoja kuharibika

BANDA LA KUPANDA UYOGA
Banda lakupandia uyoga linakuwa na sehemu  kumi na mbili sehemu ya kupandia na sehemu ya kukuzia. Sehemu ya kupandia huwa na giza chumba chote na sehemu ya kukuzia huwa na mwanga hafifu kwani  uyoga wakati unaota unahitaji carbondioxide kwa wingi na oxigyen kidogo

VIMENG'NYWE
Vimeng'nywe ni mabaki ya takataka za mazao zinatumika katika kupanda uyoga mfano , mabua ya mahindi, maranda ya mbao pamba maganda ya ndizi n.k
takataka zote za mazao zinazooza zinafaa


JINSI YA KUANDA VIMENG'NYWE
Katakata vipande vidogovidogo tayari kwa kuvianda kama shamba lako
  • Kuandaa vimeng'nywe kwa njia ya kuvichemsha kwa kutumia gunia au kapu
  • Kuanda vimeng'nywe kwa kuvichemsha kwa mvuke ndani ya mifuko ya plastiki
AINA ZA UPANDAJI
  1. Kuchanganya mbegu na vimeng'enywa
  2. kupanda kwa tabaka
  3. Kusiha mbegu juuya vimeng'enywa
MIFUKO YA PLASTIKI
Mifuko ya plastiki ndio shamba lako la uyoga inatumika kuweka vimeng'enywa na kupandia uyoga,unaweka vimeng'enywa na kupanda mbegu kisha unafunga juu na kutoboa vitundu vitano vitano kwa kila upande unapeleka katika chumba cha kupandia baada ya wiki moja au mbili uyoga utakua umeota hivyo utahamisha katika chumba cha kukuzia chana mfuko wako kwa kutumia kisu.

No comments:

Post a Comment