Labels

Wednesday 26 October 2016



Juan Mata alifunga bao lake la tatu msimu huu 

 Man Utd wawaondoa Man City kombe la EFL

Manchester United walifika hatua ya robo fainali katika Kombe la EFL baada ya kuwalaza mabingwa watetezi Manchester City kwenye debi iliyochezewa uwanja wa Old Trafford.

Juan Mata alifunga bao la pekee mechi hiyo baada ya kupata mpira kutoka kwa mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic.
Paul Pogba alikuwa amegonga mlingoti kwa kombora kali awali na kusisimua mechi hiyo kipindi cha pili.
Kipindi cha kwanza kilikuwa kikavu bila upande wowote kupata kombora la kulenga goli.
Manchester United sasa watakutana na West Ham ambao waliwalaza Chelsea 2-1.
Ushindi huo wa United ulikuwa wao wa pili katika mechi tano, na wa nne kwa Jose Mourinho katika mechi 18 alizokutana na Pep Guardiola.

Juan Mata
Image caption Mata walianza vyema kipindi cha pili

 


 

No comments:

Post a Comment