Labels

Tuesday 25 April 2017

Vita ya kuwania ubingwa Epl kuendelea leo

Wachezaji wa Chelsea
Mshike mshike wa kuwania ubingwa ligi kuu ya England utaendelea tena leo kwa mchezo mmoja kupigwa vinara wa ligi hiyo Chelsea watakua katika uwanja wao wa nyumbani kuwaalika watakatifu wa Southampton.
Nahodha wa Chelsea Gary Cahill anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi baada ya kurejea mazoezi baada ya kupona tatizo la tumbo .
Diego Costa na Eden Hazard wanatarajiwa kuanza katika mchezo huu baada ya kuanzia bechi katika mchezo wa kombe la FA dhidi ya Tottenham wikiendi iliyopita.
Mshambuliaji hatari wa Saint Manolo Gabbiadini
Kiungo wa Southampton Oriel Romeu amereje kwenye kikosi cha timu yake baada ya kufungiwa michezo miwili iliyopita, Sam McQueen is ataukosa mchezo huo akisumbuliwa na maumivu.
Chelsea wanaongoza ligi kwa alama 75 wakiwa wamecheza michezo 32 wakifuatiwa na Tottenham wenye alama 71 kwa michezo 32.

No comments:

Post a Comment